Pages

Showing posts with label Politics. Show all posts
Showing posts with label Politics. Show all posts

Thursday, June 20, 2013

Lazima nipige kura 2015

By: @Zamaradi_M

Kitambulisho changu cha kwanza kabisa cha mpiga kura! Wala sikuwa makini kiasi kwamba jina langu na la baba yangu yote yalikosewa na sikugundua!


Labda unashangaa kwa nini nimepania kupiga kura mwaka 2015, hasa ukizingatia kwamba haitakuwa mara yangu ya kwanza kutimiza vigezo vya mpiga kura!

Kadi yangu ya kwanza ya mpiga kura niliipata tarehe 17/04/2005. Nililazimishwa, na nakumbuka vizuri tulikuwa tumetoka kwenye arubaini ya Bi mkubwa nikashushwa Tabata Shule nikajiandikishe kupiga kura!

Na kupiga kura mwaka 2005 nililazimishwa pia. Sikulazimishwa nimpigie kura nani lakini kila aliyeishi na mzazi au mlezi ambaye ni polisi anafahamu hawa watu wasivyotaka utani na masuala kama haya.

Nilipiga kura, na niliipigia kura CCM kuanzia Rais hadi diwani! Niliipigia CCM kwa sababu ya shinikizo la watu waliokuwa wananizunguka kipindi kile. Kila mtu alikuwa anamuongelea Mh. Kikwete na jinsi gani atakavyopendeza na lile tabasamu lake kwenye noti. Nilichofanya ni kuchagua CCM mwanzo mpaka mwisho bila hata kuangalia majina.

Kadi yangu ya pili niliipata tarehe 03/12/2008 pale shule ya msingi Kambangwa kituo cha Kinondoni D. Hii sikulazimishwa na mtu bali na mfumo mzima wa utambulisho wa nchi hii. Kadi ya mpiga kura ni kama kitambulisho cha uraia, kwa hiyo ni lazima niwe nacho.

Na wakati huu sikuwa na Mjomba wa kunilazimisha kupiga kura kwa hiyo sikupiga kura mwaka 2010.

Sifuatilii siasa, sifuatilii kabisa! Sijui jina la hata waziri mmoja na wala sijui Makamu wa Rais anaitwa nani. Na zaidi ya yote, sioni aibu kwa hilo. Sijawahi kuwa na sababu ya kufuatilia siasa lakini sasa nina kila sababu.

Haya machafuko yanayotokea kila kukicha, yanasababishwa na nini? Kwa nini hayazuiliwi? Arusha wamepata matukio ya mabomu mara mbili ndani ya mwaka mmoja na yote ni kwenye mikusanyiko mikubwa ya watu. Watanzania tumefikia hatua ya kulipuana kwa mabomu?

Migongano ya kidini nayo! Dini zipo kabla hatujazaliwa, leo hii zinasababisha tunakosana? Kilichobadilika kwenye maandiko ya dini ni nini? Quran ni ileile na Biblia ni ileile, tatizo liko wapi? Kila dini inaelekeza jinsi ya kuishi kwa amani na majirani zako ambao sio waumini wa dini yako, huyo anayechochea chuki kwa nini hachukuliwi hatua?

Tusianze kwenye suala la rushwa! Huko ndio uozo kabisa. 

Wabunge kugeuza bunge letu tukufu sehemu ya kurushiana vijembe. Aibu gani hizi? Mbunge ni muwakilishi wangu bungeni, ikimaanisha kila anachokifanya na kuzungumza bungeni kinawakilisha matendo na mawazo yangu, nawakilishwa kweli? Je, anachokifanya mbunge bungeni ndicho ambacho 'nimemuagiza' akafanye?

Miundo mbinu! Barabara zinajengwa na kubomolewa kila siku. Nakubali nyumba ya maskini haiishi kujengwa, lakini ndio tunajenga sehemu moja kila siku? Inakuwaje kuna barabara zimedumu kwa miaka nenda rudi na nyingine hazidumu hata miaka miwili? Ndio kuna misaada ambayo inatulazimu kutumia wahandisi kutoka kwenye nchi inayotusaidia, lakini je barabara zote mbovu ni za misaada?

Wakati tunaongelea suala la kujenga, majengo yanayoporomoka nayo inakuwaje? Ukipita Ilala, Kariakoo na Posta unaona majengo yaliyojengwa hata kabla ya uhuru na bado mazima (yanahitaji rangi lakini) halafu jengo hata halijaisha kujengwa linaanguka! Ni shule na vyuo vyetu vya wahandisi, wahandisi wenyewe au wahandisi kutoka nje?

Mambo ni mengi ambayo hayanifurahishi na nataka yabadilishwe.  Na kuna mengi mazuri yamefanywa. Amani haipo kama zamani lakini pia sio vita, nashukuru kwa hilo. Mwanangu anaweza kwenda shule nzuri (baada ya mimi kulipa mamilioni ya pesa), nina uhuru wa kufanya maamuzi yangu binafsi kuanzia kwenye bidhaa gani ninunue na mambo mengine mengi tu.

Namshukuru Rais Kikwete kwa aliyoyafanya yeye na serikali yake, Asanteni sana.

Ila sitafanya makosa tena ya kupiga kura kwa kushinikizwa au kumpigia kura Rais kwa sababu atapendeza kwenye noti au kumpigia kura mgombea ambaye simjui hata jina! 

Panapo majaliwa 2015 nitapiga kura. Nitampigia kura mgombea atakayenihakikishia kutatuliwa kero zangu, kuboreshwa kwa amani na labda wenye mshahara chini ya TZS. 2,000,000 KWA MWEZI hawatakatwa kodi! Ndio, Milioni mbili! Wazungu wanasema a girl is allowed to day dream (msichana anaruhusiwa kuota ndoto za mchana)!

Wewe utapiga kura 2015? Utampigia kura nani na kwa nini?


MUNGU IBARIKI TANZANIA, MUNGU TUBARIKI WATANZANIA.

Friday, June 14, 2013

Tumfunge Paka Kengele

By: @Zamaradi_M



Kuna hadithi nilihadithiwa wakati nakua. Nje kidogo ya kijiji ambacho wakazi wake wote walikuwa panya kulikuwa na paka ameweka makazi. Paka yule aliwavizia panya nyakati za usiku na kuwala. Panya wakafanya kikao na katika majadiliano wakaona njia ya kupambana na adui yao ni kumfunga kengele, ili akiwa karibu basi wamsikie. Ila, nani atamfunga paka kengele?

Kwenye hili janga la madawa ya kulevya linaloikumba nchi yetu, lazima huyu paka tumfunge kengele. Tatizo ni kwamba, akienda panya mmoja tu ni rahisi kugeuzwa mlo. Ila tukiwa wengi, hata kama wengine tutakuwa mlo tutashinda vita. Tutaacha kijiji chetu kikiwa salama, ndio ushujaa huu tuliokuwa tunauimba enzi zile za mchakamchaka.

Suala la madawa ya kulevya! Tofauti na matatizo mengine ambayo hata pa kuanzia hamna, hili liko waziwazi. Waathirika tunawaita mateja, wamejaa karibu kila kituo cha daladala Dar es Salaam, vijiwe vyao vinajulikana kabisa. Na ukiwaona wala huhitaji teknolojia ya hali wa juu kuwatambua, wana alama zao usoni. Waangalie vizuri midomo na wasikilize wakipiga debe!

Kwa machache tu niliyoyaona kwenye filamu za kipelelezi najua kupata mwanzo mzuri kama huo ni ishara ya kuwa na kesi itakayofika mwisho. Tunashindwa nini kuanzia hapo? Tunashindwa nini kufuata huo mnyororo mpaka tukawafikia hao wahusika wakubwa? Na kama kisingizio ni wao kuwa na ushawishi na fedha nyingi basi huo ni udhaifu kwa serikali yetu.

Naelewa vyema kwamba hatuwezi kumaliza vita dhidi ya madawa ya kulevya kwa asilimia mia moja, ila hali mbaya kwa sasa. Tupunguze kwa hizo asilimia tutakazoweza. Na hata kama wataendelea kuuza na kutumia basi iwe kwa siri. Hii hali ya mateja kuwepo hadharani ni kashfa kubwa sana kwa serikali na wahusika wote.

Kweli tumefikia hatua ya watu kuvunja sheria bila uoga? Nani asiyejua kwamba kuuza na kutumia madawa ya kulevya ni kosa? Kwa hiyo anayetumia na kuonesha kwamba anatumia ni kwamba anaikebehi serikali, jeshi la polisi na kila aliye kwenye vita dhidi ya madawa ya kulevya? Ni kama vile wanatuambia, 'Ndio nauza na natumia, unasemaje sasa?'

Na suala lingine, kumekuwa na habari kuhusu watanzania waliokamatwa nje ya nchi wakisafirisha madawa ya kulevya. Kulikuwa na yule dada aliyekuwa anyongwe, niliacha kufuatilia baada ya kuona picha yake na mwanae kwenye sintah.com. Na pia kuna kaka ambaye amehukumiwa kwenda jela miaka nane nchini Angola na hii nimeiona kwa millardayo. Huyu aliyeko Angola anaomba arudishwe Tanzania kwa sababu mazingira ya Angola ni magumu.

Tuweke hisia pembeni, hawa wanaosafirisha madawa ya kulevya wanafanya hivyo kwa faida zao binafsi, na  hata kodi hawalipi! Leo amekamatwa serikali iingilie kati, itumie kodi zetu ili warudishwe nchini! Na mbaya zaidi eti mazingira ya jela za kule ni mabaya! Samahani, kama nina maamuzi na kodi yangu naomba isitumike huku. Anayetaka basi atoe hela yake. Angefanikiwa kufikisha huo mzigo angefaidika yeye na familia na rafiki zake, basi na wamsaidie sasa.

Na angefanikiwa kufikisha huo mzigo, ungeua na kutesa vijana wangapi? Huo mzigo anaouleta yeye ndio unasababisha tukwapuliwe vijipochi na visimu vyetu kila siku! Tunaishi bila amani. Tunapoteza nguvu kazi ya taifa kwa sababu tu kuna watu wachache wanataka maisha mazuri na ya harakaharaka. Hata mimi nayatamani ila najua hatari yake, sio tu kwangu bali kwa mwanangu, ndugu jamaa na marafiki. Ndio maana nimeamua kutokuwa mbinafsi na kutafuta hela yangu kihalali. Kwa nini nilipe kwa makosa na maamuzi ya watu wengine?

Sikubaliani na adhabu ya kifo, kwa hili kodi yangu itumike. Itumike kuokoa maisha ya huyo muhalifu. Na kama atarudishwa nchini, awekwe jela ikibidi kifungo cha maisha.

Ni wakati sasa kila mtu awajibike kwa makosa yake. Tuache kuoneana aibu na kuoneana huruma zisizo na sababu. Kuna msemo wa kizungu unasema you've made your bed, now you'll have to lie in it (Umetandika mwenyewe kitanda chako, itabidi ukilalie). Sasa kama hukutoa wale kunguni hilo halituhusu.

Haya, nani yuko tayari kumfunga paka kengele?

Nimeandika makala hii kama njia ya kumuenzi Langa. Moja ya vipaji adimu tulivyobahatika kuvishuhudia. Mpaka mauti yanamkuta Langa ambaye alikiri kuwa muathirika wa madawa ya kulevya alikuwa katika vita dhidi ya kilevi hicho hatari.

Tangulia Langa, tupo nyuma yako.

Thursday, May 23, 2013

Will I die for my country?

By: @Zamaradi_M




On our way to work with some colleagues we were talking about the current events. And nothing is more 'current' now than the Mtwara unrests. When it comes to politics I am just a tiny step above those who still believe that Mwalimu Nyerere is the president of this beautiful nation.

My point is, I do not know the political side of this issue or of any issue for that matter. What I have heard is that the citizens of Mtwara are protesting against the government's decision to build a gas pipe that will transfer gas from Mtwara to DSM where it will be processed.

These protests went as far as burning government buildings, torching cars that are owned by the government employees (I hope their insurance covers this) and worst of all people have lost their lives and some keep endangering their lives. This got me questioning, if it comes down to it, will I willingly die for my country? Will YOU willingly die for your country?

Depends, if they take all corrupt politicians and put them in one stadium (I am not sure they can fit anywhere else) I will happily wear a bomb and go with them. But wait, we can just put the bomb in the stadium, close the doors and save one good person. As Devi would say, why should bad things happen to good people?

And make no mistake though, if the country is invaded and I have to fight to save lives, I will fight.

May be I am a coward, a traitor, a disgrace to this lovely nation, but if I am to be honest, I will not die for my country. Besides, the after life freaks me out!

I respect the people who will and who have lost their lives in the names of their countries. I admire their courage and their unselfishness.

I think of dying for my country and I ask myself, who will take care of Mama Mkilalu? Will my fellow patriots look after my 3years old Tanisha? Will this country that I died for make sure she gets a decent education and a chance to a better life?

And then I ask again, what will my death accomplish? Will it be just another statistic? Will those corrupt leaders resign, or better yet commit suicide because I died for my country?

So. all these questions whose answers we will never know got me saying NO to dying for my country. It is just too much of a risk. I love my country. Instead of dying for it I'd rather stay alive and fight.

Why don't we go to school, study whatever it is we need to study and fight for our country in the safest way possible. And if we have to protest why don't we do it in a way that we will all stay alive long enough to see our children grow up and our parents enjoy their uzee?

Call me selfish and all the names you can think of but if I have a say in it, I will not die for my country kwa kweli. I just don't see the point.